Thursday, March 7, 2013

DIAMOND ATINGA SEDUCTIVE KWA MR. TOUCHEZ

Jana Niliweza kupata appointment ya kuingia Studio za Seductive Records pale Mitaa ya Mikocheni Viwandani karibu na kituo cha ITV cha mabasi.

Cha kwanza nilikaribishwa na Walinzi walio makini na kujiandikisha katika kitabu cha wageni na kisha kusachiwa kama kuna chochote kibaya nimebeba then nilipewa go ahead na kuelekea moja kwa moja katika mapokezi nako nilipokewa kwa smile na kusubiri kidogo kwa ndani bado jamaa walikuwa wakipiga kazi.

Baada ya kama nusu saa ndipo sauti tamu ya dada wa mapokezi ilisikika ikisema welcome to seductive na naamini wewe ni mgeni wa T......, nami niliitikia kisha nikajuwa naingia ndani, kumbe ilikuwa ni maswala ya drinks nk nami nikaona safi nikaagiza joice baridi.

Haikupita mda mrefu nikasikia sauti ileile ikiniita tena niingie Studio Lab, ndipo nami nikajisukuma fasta.

Nilipokewa kwa uchangamfu na Mr. T touchez ( Producer ) kisha kukaa kimya na kuangalia jinsi gani mambo yanavyo kwenda katika upikaji wa Single ambayo ni gumzo la mji kwa sasa ya Diamond na Nay.






Wednesday, February 20, 2013

KICHUPA KIPYA TOKA KWA OCHU SHEGGY


Studios za Emptysoulz Production zimeondoa ukimya toka swala la kuhama toka Analog kwenda Digital kuharibu mipango mingi haswa kwa Wasanii, Makampuni mbalimbali na jamii nzima.

Akiongea kwa njia ya simu The C.E.O na Diretor wa Studio hizo bwana Solomon Lamba alilonga na Kazikali kuwa kazi inayotoka kwa sasa ni ya Ochu Sheggy inayokwenda kwa Jina la Kingereza akiwa amepewa mkono na mwanadada Aneth.

Muzic Video hiyo ambayo imefanyika nje ya mji ili kubadili muonekano ili kwenda sawa na Story nzima imeshakamilika na soon wengi wataishuhudia kazi hiyo makini.












Tuesday, February 12, 2013

SIRTINO AKESHA SEDUCTIVE RECORDS


Msanii Sirtino yupo mbioni kutoa Track yake mpya atakayemshirikisha Mr. Blue a.k.a Baisa
Sirtino kwa sasa anaetesa na Single yake ya 2lia haswa katika Luninga amesema watu wakae mkao wa ujio mpya kwani Producer wake Mr. T Touchez amempa kazi kubwa sana kwa kumpa Beat kali hivyo ni lazima aitendee haki Beat hiyo kwa Vocals zenye kumtoa nyoka pangoni.
DIRECTOR WA KITAMBO


Ukisikia kina TMK Wanaume, Dully Sykes ,  Juma Nature, Matonya , Yp , Ydash, Chidi Benz, Tunda man, Madee, Chege na Temba na wengine wengi.... Basi huyu jamaa kapiga Videos kitambo na Mpaka sasa anaendelea gonga Vichupa vikali kwenda mbele.

Kwa jina anaitwa Solomon Lamba na ndiye C.E.O wa Studios za Emptysoulz Production zilizopo Mikocheni karibu na kituo cha mabasi cha ITV.

Ameshawahi beba Kili Awards mara mbili na nyingine toka nje ya nchi, kwa sasa anapiga si kazi za Music Videos tu bali mpaka Tv Programes, Documentarys, na soon anaingia upande wa Movies.

Kazikali imeona si haki kama haitampongeza Director huyu kwa Mchango wake mkubwa ktk Bongo Fleva na Sanaa kwa Ujumla.